KISWAHILI

MABADILIKO YANAYOUMIZA NDANI YA KANISA

Book information

Publisher
Truth Printing Press
Year
2020
ISBN
9789976572629
Language
kiswahili
Format
PDF
Filesize
749 kB (766864 bytes)
Series
Kitabu katika nyanja ya utawala wa kanisa
Edition
1
Pages
81\81
Time added
2021-04-06 03:34:42

Description

Katika mataifa ya mengine siku hizi huwezi kuwa mchungaji wa kanisa linalojitambua ukiwa huna angalau Elimu ya Sekondari na kumaliza seminari. Katika nchi zingine, uchungaji imeorodheshwa kuwa mojawapo ya kazi zinazotambuliwa ndani ya serikali. Ni mojawapo ya kazi ambayo mtu lazima awe na maarifa ya Mungu na ya kidunia. Kinyume chake, katika mataifa mengine, mtu akiweza kunena kwa lugha tu, anakabidhiwa kundi. Ndiyo! Naamini katika uongozi wa Roho Mtakatifu katika kuongoza kanisa; wenye elimu na wasio na elimu ni sawa tu. Na wakati mwingine wasio na elimu yoyote wanaweza kuongoza kanisa vizuri kuliko wenye elimu. Hata hivyo, itakuwa ni kazi kubwa sana yenye kuchosha, kwa sababu mambo mengi unaweza kuyafanya kama uko gizani. Kwa kuzingatia uhitaji wa elimu ya uongozi ndani ya kanisa; uwe na elimu, ama usiwe na elimu, kitabu hiki kinakufaa kwa sababu nimekiandika katika mazingira ya uzoefu na mazoezi; kitamsaidia kiongozi yeyote ndani ya kanisa kuwa mwajibikaji ikiwa ataamua kukitumia vizuri, na kufuata maelekezo yake. Katika kitabu hiki, nimejaribu kujadili kwa kina mambo muhimu ambayo mtumishi wa Mungu akiyafanya ndani ya kanisa kuna uwezekano mkubwa wa kubadilisha kundi lake. Nimezungumzia mabadiliko ya kulifanya kanisa liwe ni kanisa hai mbele za Mungu likiwa linatimiza Utume Mkuu. Ni kweli kwamba Mungu ndiye huleta mabadiliko ndani ya kanisa, lakini ukweli huu hauondoi jukumu la kiongozi wa kanisa; mchnungaji, mzee, mwinjilisti, shemasi, mkuu wa idara, pamoja na kila muumini ndani ya kanisa. Pamoja na juhudi kubwa za viongozi wa kanisa, kuna uhitaji wa kanisa zima kushiriki katika shughuli za maendeleo ya kanisa, ili kanisa likue kwa pamoja. Mch. Daniel John Seni Shekinah Presbyterian Church in Tanzania, Dar es Salaam Desemba, 2020 Historia ya Mwandishi Daniel John Seni, ni mchungaji. Alimuoa Esther Mligo mwaka 2011. Alizaliwa miaka 40 iliyopita katika wilayani Meatu, Mkoani Simiyu Alisoma katika shule ya Msingi Tindabuligi kati ya Mwaka 1990-1997. Baada ya kumaliza elimu ya msingi, hakupata alama za kutosha kuruhusu aende sekondari, na badala yake aliendelea kujishughulia na shughuli za kilimo nyumbani kwao Tindabuligi kuanzia mwaka 1997-2002. Mwaka 2002 alipata wito wa kumtumikia Mungu na alitumika chini ya kanisa la Africa Inland Church Tanzania (AICT) kama mwinjilisti, kijijini kwao. Na mwaka 2003 alienda kusoma katika chuo cha Biblia Kolandoto (Kolandoto Bible School) kilicho chini ya Kanisa AICT. Akiwa chuoni, alikutana na Mmissionari kutoka Korea Mwl Boyeon Lee, ambaye aliamua kufanya kazi pamoja naye. Na kuanzia hapo, alianza kujiendeleza kwa kusoma elimu ya watu wazima na kufanya mtihani wa QT mwaka 2005. Desemba 2005, alihamia Dar es salaam, na baadaye mwaka 2006, alijiunga na chuo cha Calvin Theological College, (CTC) kilicho chini ya Korea Church Mission Tanzania (KCM). Akiwa anaendelea na masomo ya Theologia, huku akijiendeleza na masomo ya watu wazima, mwaka 2007 alifanya mtihani wa Kidato cha Nne, na mwaka 2010 alifanya mtihani wa kidato cha Sita. Mwaka 2013 alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es salam na kusoma kozi ya BA.Kiswahili, na kuhitimu mwaka 2015. Mch. Daniel J. Seni alisimikwa kuwa mchungaji rasmi katika kanisa la Presbyterian Church in Tanzania Julai 2014. Mwaka 2016 alijiunga na chuo kikuu cha Chongshin Theological Seminari nchini Korea Kusini kwa ajili ya shahada ya Uzamili, na kuhitimu mwaka 2019 alihitimu. Mwaka 2020 alijiunga na Chuo cha Calvin Graduate School of Theology nchini Korea Kusini kwa ajili ya kusoma kozi ya Shahada ya Uzamivu, ambapo mpaka sasa bado ni mwanafunzi. Mch. Daniel J. Seni kwa sasa ni mchungaji kiongozi wa kanisa la Shekinah Presbyterian Church in Tanzania. Mch. D.J. Seni ni mwandishi wa vitabu vifuatavyo 1. Uwezekano wa Mkristo Kupagawa pepo 2. Upandaji wa Makanisa 3. Tamthiliya ya Mzee Maduhu 4. An anaysis of Westimister Confession of Faith: Pneumatological Approach (amazon) 5. The Inevitability of Women’s Ordination (amazon) 6. Dhana ya Mafanikio 7. Namna unabii wa Media unavyokinzana na Nabii za Kibiblia (Amazon) 8. Njoni Tuabudu: Taratibu za Ibada Hivi karibuni amejikita katika uandishi wa vitabu vya mafundisho ya msingi ya kanisa (Church Doctrines) na miswada iliyo tayari ni:- 1. Ekklesiolojia 2. Anthropolojia 3. Soteriolojia 4. Eskatolojia Mch. Daniel J. Seni ametafsiri katika Kiswahili vitabu vifuatavyo:- 1. The Westminster Shorter Catechism 2. The Westminster Larger Catechism 3. The Westminster Confession of Faith YALIYOMO Tabaruku i Utangulizi ii YALIYOMO iii SURA YA KWANZA 1 TAMBUA DHANA YA KUPINDUA ULIMWENGU 1 SURA YA PILI 8 TAMBUA AINA YA WASHIRIKA ULIO NAO 8 1. Washirika Wanaokataa Uhalisia wa Kanisa lao 9 2. Washirika waliojikinai 11 3. Washirika walalamikaji 12 4. Washirika wakosoaji 14 5. Washirika Walioridhika na Hali ya Kanisa 15 6. Washirika Tegemezi 17 SURA YA TATU 19 TAMBUA MAMBO YA MSINGI KUANZA NAYO 19 1. Maombi Yasiyokoma 19 2. Fikiria mambo makubwa kuliko uwezo wako 21 3. Kubali Ukweli na Ukabili Ukweli 25 4. Jifunze kwa Wengine. 31 5. Kubali Kulipa Gharama 32 6. Pambana na Tabia Zinarudisha Maendeleo 37 7. Kuwa Sauti ya Matumaini na Maono 42 8. Tarajia Upinzani Kwenye Mabadiliko 48 9. Shughulika na Mahitaji ya Watu 53 10. Kuthamini Watu Wanaokuunga Mkono 58 11. Kubali bila Majuto wengine Waondoke 59 12. Zingatia Uwezo wa Washirika 61 13. Mfanye Kila Mshirika Awe Shahidi 62 Historia ya Mwandishi 72

Similar books